Zuchu Nimechoka Lyrics
Umenijengea kumbukumbu mbaya kwenye penzi lako
Siwezirudi haat nishikie bakora
Nanena kwa machungu umentendea vibaya mi, mwana mwenzako
Kwa makusudi furaha imeniporaa
Aah, asante umenifunzaa
Nionapo njia nichagua yakuvuli
Mimi, mi sio wa kwanza kuumizwaa
Wanatendwa matajiri, sembuse mi hula sifuri
Aah, na nakujua kwa msingizia she kwani
Huyo ni wewe, ni wewe, ni wewe
Ukinikumbuka usijipigishe u-turn
Uniache mwenyewe, mwenyewe, mwenyewe niache
Nimechoka, nimechoka
Nimechoka, baasi
Nimechoka, nimechoka
Nimechoka, baasi
Eh, hasira
Hasira ndo maradni yangu
Hasira
Nimepoteza muda wangu jamani hasira
Hasira ndo ugonjwa wangu
Hasira
Nimepoteza lingo langu
Sitamani sitamani makosa niyarudie
Isiwe desturi yangu kuuchuza moyo uumie
Bora nirudi nyumbani Pemba wanitambikie
Nifungwe akili yangu, mawazoni nikutoe
Ooh maana nakujua kwa msingizia she kwani
Huyo ni wewe, ni wewe, ni wewe
Ukinikumbuka usijipigishe u-turn
Uniache mwenyewe, mwenyewe, mwenyewe niache
Nimechoka, nimechoka
Nimechoka, baasi
Nimechoka, nimechoka
Nimechoka, baasi